TUNAKUTHAMINI TUNAKUPENDA NI FAHARI YETU KUKULETEA TAARIFA MBALIMBALI KUTOKA SEHEMU TOFAUTITOFAUTI ZA DUNIA KUWA MJANJA KUPATA TAARIFA MAPEMA
**IJUE DUNIA YAKO MAPEMAAAAAA**
RIWAYA YA KISWAHILI NUKUU ZA SOMO: MAANA YA RIWAYA NA AINA ZA RIWAYA: Riwaya imefasiliwa na wataalamu mbalimbali miongoni mwao nikama vile, Encyclopedia Americana (EA), Jz. 20 (1982:510f) wakinukuliwa naMulokozi (1996) wanasema, riwaya kuwa ni hadithi ya kubuni inayotosha kuwa kitabu. Udhaifu; Maelezo haya yanaibua utata kwani hayafafanui kitabu kinapaswa kuwa na urefu kiasi gani. Matharani kwa mujibu wa UNESCO katika Mulokozi (1996) kitabu ni chapisho lolote lenye kurasa 48 au zaidi. Ama urefu wa kitabu hautegemei idadi ya kurasa tu pia unategemea ukubwa wa kurasa (upana na kina) ukubwa wa maandishi na mpangilio wake. Encyclopedia Britanica EB, Jz.8, (1985:810) wakinukuliwa naMulokozi (1996) wanaeleza kuwa, riwaya ni masimulizi marefu yakinathari yaliyochangamana kiasi, yenye kuzungumzia tajriba ...
Daniel Seni Academia.edu KI 311 SEMANTIKI NA PRAGMATIKI YA KISWAHILI DOWNLOAD 27 Seni, Daniel John/ An ordained pastor at Shekinah Presbyterian Church (T) Madale-/DSM. Contact him through +255769080629/+255786684062 or senishekinah@gmail.com 27 Mfano wa maswali; Familia yenu ina watu wangapi? Mbali na Wamasai ni watu gani wengine wanaojihusisha na ufugaji? 2. Matendo uneni yasiyo dhahiri Haya ni matendo ambayo aina ya sentensi haiwiani bali inakinzana. Kwa mfano:- Unaweza kumkopesha shilinga elfu kumi — sentensi hii kimuundo ni swali lakini dhima ni ombi. Kwa hiyo inafanya tendo uneni lisilo dhahiri. Mfano mwingine Njaa inaniuma sana — kimuundo sentensi hii inatoa inatoa taarifa lakini dhima ni kuomba chakula. Kwa hiyo katika muundo huu ni kuwepo kwa muundo tofauti na dhima. Aina za Matendo Uneni Austin (1962) ametaja aina tatu:- 1. Kile kisemwacho Aina hii inahusu usemi wa sentensi yoyote yenye maana inayoeleweka pia iwe na kitu kinachorejelewa. 2. Lengo...
Ushairi wa Kiswahili waweza kuainishwa katika tanzu au kumbo mbalimbali. Mulokozi (1996), ameuainisha ushairi wa kimapokeao katika kumbo kuu tatu za kimtindo. Kumbo hizo ni: ushairi wa kijadi au kimapokeo; ushairi wa mlegezo; na ushairi wa maigizo. 1. Ushairi wa Kimapokeo Haya ni mashairi ya kijadi yenye kufuata kanuni za urari wa mizani na mpangilio wa vina vya mwisho na/au vya kati. Mfano wa shairi la kimapokeo ni huu hapa: Namshukuru Namshukuru Illahi, Mwenyezi mkamilifu, Kwa kuishi nikawahi, kazini kustaafu, Bado ningali sahihi, imara na mkunjufu, Alihamdulilahi, namshukuru Latifu. Ulimwengu wa rakadha, umejaa hitilafu, Sikuweza mambo kadha: karibu mambo elfu; Kanipa hii karadha, Bwana Mungu namsifu, Alihamdulilahi, namshukuru Latifu. Hii sikutazamia, kwamba litanisadifu, Bahati imenijia, kwa kupenda Mtukufu, Mfano kama ruia, Mungu hana upungufu, Alihamdulilahi, namshukuru Latifu. (Shaaban Robert, 2003: 102 – 104) 2. Ushairi wa Mlegezo Haya ni mashairi...
Maoni
Chapisha Maoni
Tafadhari usicomment matusi